Social Icons

Featured Posts

Monday 4 April 2022

HAKUNA CHAMA CHA MTU LAZIMA TUSIMAMIE HAKI. KINANA



Ndugu Abdulrahman Kinana Makamu Mwenyekiti CCM Tanzania bara


Na Janeth Raphael - Dodoma

Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa wamepiga kura ya kumuidhinisha Mgombea wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho

Hayo yamefanyika kwenye Mkutano Mkuu wa CCM uliofanyika Leo April 01, 2022 Jijini Dodoma ambapo Katibu Mkuu Mstaafu wa Chama cha Mapinduzi CCM Abdulrahman Kinana ameshinda kiti hicho kwa Kura zote 1875 zilizopigwa na Wajumbe ambazo ni sawa na Asilimia 100%

Akizungumza baada ya kushinda Abdulrahman Kinana alimshukuru Mwenyekiti wa Chama hicho Mhe. Samia Suluhu Hassan

“Juzi uliniita nikawa najiuliza nimeitiwa nini, nikajua ni katika kusalimiana.Rais akaniambia nataka uwe Makamu Mwenyekiti, nikamwambia sina hiari, sina budi kukubali, napenda kukuhakikishia Mwenyekiti nitajitahidi kadri ya uwezo wangu kufikia matarajio yako, Niseme sitokuangusha”

Kinana aliishukuru Kamati Kuu kwa kupitisha jina lake, pamoja na wajumbe wa Halmashauri kuu kwa kupitisha na kuidhinisha jina lake

“Mmenipa imani kubwa, na mimi nitakitumikia Chama changu, wana CCM na Watanzania”

Alimshukuru Mzee Mangula ambapo alisema amejifunza mengi kutoka kwake na kumpongeza kwa kustafu kwa Heshima

“Kama Mangula asingeamua kustaafu, basi leo nisingekuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi”

Makamu Mwenyekiti Kinana aliwashukuru Wenyekiti wote kuanzia Baba wa Taifa mpaka sasa Rais Samia Suluhu Hassan na kusema kuwa mengine ni mapungufu yake mwenyewe

Aliahidi kwenda kusimamia Chama kuwa imara Kidemokrasia na kusimamia haki ya kuchaguliwa bila upendeleo

Alisema haki nyingine ni kutoa Mawazo

“Lazima wanachama wawe Huru kutoa mawazo, hakuna mwenye hakimiliki ya mawazo, lazima tumsikilize kila mwananchi, na wanachama wakimchagua mtu kwani sisi ni nani wa kupinga”

Alisisitiza kusimamia Demokrasia na kusema ni lazima kusimamia haki

“Nimekuwa nikimsikia Rais akisisitiza mara zote katika kusimamia haki, nilimsikia akisema Vyeti peke yake siyo sifa, Vyeti viende na uadilifu, kukubalika, Nchi hii inajulikana kwa Haki ndani na nje ya Nchi”

Alisema jukumu lake la Tatu ni kwamba CCM si mali ya Serikali ila Serikali zinatokana na CCM ambapo alieleza kuwa CCM haipokei maelekezo kutoka Serikalini

“CCM haiagizwi na Serikali, CCM Inaagiza Serikali, na wanaokwenda kuomba kura ni CCM sio Serikali, niwasihi Viongozi wetu msitudhulumu hiyo haki”

Alisema Serikali inapokuwa na mapungufu wenye jukumu la kuzisemea kasoro ni Chama

“Na hatutazisemea kwa kukejeli, tutaitana kwenye Vikao vyetu vya Ndani, si sawa kwa Mwana CCM kwenda hadharani kuisema vibaya Serikali yake”

Kinana alisisitiza, Chama cha Mapinduzi ni kikubwa na kinakubalika hivyo ni lazima CCM ibaki kuwa masikio kwa Wananchi

Aliahidi utumishi uliotukuka ili Chama kuendelea kuwa imara na umoja

“Hili nalo ni la umhimu, nataka niwasishi hakuna chama cha mtu, kuna Chama cha Mapinduzi.ndani ya hiki chama hakuna ukanda, haya mambo ya ukanda, ukabila, udini tukae nayo mbali.mtu akikosa hoja, maarifa anaingia kwenye kichaka cha udini, ukabila, ubara na visiwani.hiyo si sawa kwa chama hiki, tunaweza kutofautiana kwa sababu nyingi lakini siyo kikanda au kikabila

Athman Hemed Sampa afariki dunia

Aliyekuwa Diwani wa Kata ya Busale Wilayani Kyela Mhe. Athman Sampa amefariki dunia katika hospital ya Rufaa Mbeya. Marehemu Sampa kabla ya kuwa Diwani alishi nyazifa mbali mbali katika Chama Cha Mapinduzi zikiwemo, Mwenyekiti UVCCMwilaya ya Kyela, Mjumbe Kamati Siasa Mkoa Mbeya, Katibu Mwenezi Wilaya ya Kyela n.k

Mwenyezi Mungu aiweke roho ya marehemu Athman Hemed Sampa mahala pema peponi Amina.

Sunday 18 March 2018

WATUMISHI WA AFYA WAASWA KUJIEPUSHA VITENDO VYA RUSHWA SEHEMU ZAO ZA KAZI

NA WAMJW-DAR ES SALAAM


WATUMISHI wa sekta ya Afya nchini wametakiwa kujiepusha na vitendo vya kutaka rushwa kutoka kwa wananchi wanapokuwa sehemu zao za kazi ili kuendana na maadili ya utumishi wa Umma. 

Hayo yamezungumzwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto katika kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo kilichofanyika leo jijini Dar es salaam ili kujadili mustakabari wa utoaji huduma za Afya nchini. 

“Marufuku Watumishi wa sekta ya afya nchini kujiingiza kwenye vitendo vya rushwa na kama wapo naomba waache mara moja kwani atakayebainika anajihusisha na rushwa sheria itafuata mkondo wake mara moja” alisema Waziri Ummy. Aidha Waziri Ummy amesema kuwa watumishi wa sekta ya afya hasa katika sehemu ya kutolea huduma za afya wanatakiwa kuwa na lugha nzuri kwa wananchi pindi wanapotoa huduma sehemu zao za kazi. 
aziri Wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akifungua Mkutano Wa Balaza la Wafanyakazi Wa Wizara ya Afya mapema leo Jijini Dar es salaam.
Mganga Mkuu Wa Serikali Prof. Muhammad Bakari Kambi akimkaribisha mgeni rasmi Waziri Wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu(hayupo kwenye picha)
Mkurugenzi Wa Mafunzo na Rasilimali watu Dkt.Otilie Gowelle wakwanza kulia akifuatilia kwa makini maagizo ya Waziri Wa Afya Mhe.Ummy Mwalimu katika mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Afya uliofanyika jijini Dar es salaam.
eza kuu ikiongozwa na Waziri wa Afya Mhe.Ummy Mwalimu na mganga Mkuu wa Serikali Prof. Kambi wakati wakiimba wimbo wa kuhamasisha umoja na mshikamano kwa Wafanyakazi, pindi wakifanya mkutano wa Baraza la Wafanyakazi, Wakwanza ni Katibu wa Baraza hilo Mary Ntira na wa mwisho ni Afisa Elimu kazi na mratibu wa Jinsia taifa TUGHE Bw. Nsubisi Mwasandende
Watumishi wa Wizara ya Afya wakiongozwa na Mkurugenzi wa Tiba Dkt. Dorothy Gwajima wapili kutoka kulia.
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu katikati waliokaa akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa Baraza la wafanyakazi kutoka Wizara ya Afya mara baada ya kikao cha Baraza hilo kilichofanyika Leo jijini Dar es salaam.


Chanzo. Michuzi blog

Urusi yashutumu mataifa ya Magharibi

Urusi imeyashutumu mataifa ya Magharibi kwa kuwasaidia waasi nchini Syria, baada ya mkutano na Iran na Uturuki kwenye awamu ya mazungumzo mapya ya kujaribu kutafuta ufumbuzi wa mzozo unaoendelea nchini humo.

Kasachstan Syriengespräche in Astana (Reuters/M. Kholdorbekov)

Mawaziri wa mambo nje wa Urusi, Iran, Uturuki walikutana katika mji mkuu wa Kazakhstan, Astana, wakiangazia suala la Ghouta Mashariki ambayo ni ngome ya upinzani iliyoko nje ya mji wa Damascus, iliyoanza kushambuliwa mwezi mmoja uliopita na utawala wa rais Syria Bashar al-Assad.

Mkutano wa Astana ulilenga kuweka msingi wa kikoa cha marais wa mataifa hayo matatu kitakaochofanyika mjini Istanbul Aprili 4. Akiongea baada ya mazungumzo hayo waziri wa masuala ya kigeni wa Urusi Sergei Lavrov ameyalaumu Mataifa ya Magharibi kwa kuwakingia kifua waasi na hata kuimarisha uwezo wao wa kivita.

Mataifa ya Urusi na Iran yanamuunga mkono rais Assad, lakini Uturuki imetaka kusitishwa kwa mashambulizi Ghouta Mashariki ambapo takriban watu 1,260 wameuawa wengi wao wakiwa watoto tangu lianze kushambuliwa mwezi Februari tarehe 18.

Syrien Luftangriffe auf Ost-Ghuta (picture-alliance/abaca/AA/M. Taim)

Syria yashambulia eneo la Ghouta Mashariki

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelielezea janga la kibinadamu katika eneo hilo ambalo halina chakula, maji na mahitaji mengine ya kimsingi kuwa jehenamu ya duniani.

Lavrov ayakosoa mataifa ya Magharibi

Lakini  Lavrov alisema kuwa mtazamo wa mataifa ya Magharibi ni wa upande mmoja na kuwashutumu wenzao kwa kujaribu kuwalinda waasi, akitoa mfano wa kundi la Hayat Tahrir al-Sham ambalo limeundwa na waliokuwa wapiganaji wa kundi la Al-Qaeda ambalo liko Ghouta Mashariki. Amesema kuwa kundi hilo linafuata maelekezo kutoka kwa mataifa ya Magharibi. Lavrov pia ameonya dhidi ya kitisho cha Marekani kuushambulia mji mkuu wa Syria Damascus haitakubalika.

Lavrov amesema, "tunapenda kukumbusha kwamba matumizi ya nguvu dhidi ya Damascus kwa visingizio hayakubaliki. Vitisho vilivyotolewa hivi karibuni na Marekani kuhusu mashambulizi ya upande mmoja dhidi ya Syria ikiwemo Damascus - kama tuhuma zisizo na msingi mwezi Aprili mwaka uliopita kuhusiana na matumizi ya silaha za kemikali na serikali ya Syria - hazikubaliki na hazitovumiliwa."

Urusi, Iran na Uturuki zaafikiana

Katika mwafaka uliotiwa saini na Lavrov, Mohammad Javad Zarif wa Iran na Mevlut Cavusoglu wa Uturuki- na kutolewa na wizara ya mambo ya nje ya Kazakhstan, mwishoni mwa mazungumzo, mataifa hayo matatu yaliamua kuvunja nguvu za makundi yanayohusishwa na Al-Qaeda.

Ghouta Mashariki ilistahili kulindwa na kuwa salama. Lakini utawala wa Syria na Urusi wametumia kisingizio cha waasi katika eneo hilo kutekeleza mashambulizi.  

Wakati hayo yakiarifiwa shirika la uangalizi wa haki za biadamu nchini Syria linasema mashambulio ya angani ya Urusi na serikali ya Syria Ghouta Mashariki yamesababisha vifo vya watu wasiopungua 46 katika muda wa masaa 24.

Türkei beginnt Offensive Operation Afrin in Syrien (picture alliance/AA/O. Coban )

Eneo la Afrin lashambuliwa na utawala wa Syria

Ripoti ya kundi hilo inasema kuwa mji wa Kafr Batna ulishambuliwa na vilipuzi hii leo. Vikosi vya serikali  vinaelekea katika ngome za waasi hali ambayo imechangia raia wengi kuhama.

Kwingineko katika mji wa Afrin ulioko kaskazini mwa Syria takriban raia 20 wameuawa, miongoni mwao kina mama na watoto huku wengine 30 wakijeruhiwa.

Picha zilizotumwa na wanaharakati wa Kikurdi zilionyesha watoto wakilia huku wakitokwa damu walipokuwa wakipelekwa katika hospitali ya Afrin kutibiwa.

Chanzo. Dw.de


Ujerumani sasa ina serikali mpya

Wahariri wa magazeti ya Ujerumani wamejishughulisha zaidi na mzozo kati ya Uingereza na Urusi kuhusiana na shambulio la sumu dhidi ya jasusi wa zamani wa Urusi nchini Uingereza, na pia kuhusu serikali mpya ya Ujerumani.

Deutschland Ernennung des neuen Bundeskabinetts (Reuters/F. Bensch)

Mhariri wa  gazeti  la Rhein-Zeitung  la  mjini  Koblenz  anaandika kwamba uchaguzi mwingine  wa  majimbo utaonesha iwapo kile kinachoonekana  kuwa ni kuaminika  na  wananchi  kwa  muungano wa  vyama vya  kihafidhina  na  SPD kuunda  serikali kumefanikiwa. Mhariri  anaendelea.

Mtihani wa  kwanza  utakuwa  mnamo wakati  wa  kuelekea mwishoni  mwa  mwaka  huu katika  jimbo  la  Bavaria  na  kisha Hesse. Mwaka 2019 kutakuwa  na  mtihani  mwingine  wa uchaguzi wa  bunge  la  Ulaya  na  kisha  uchaguzi  katika  majimbo  matatu ya mashariki  mwa  Ujerumani. Hali  itakwenda  vizuri , iwapo  vyama ndugu  vya  CDU /CSU  pamoja  na  SPD  hadi  wakati  huo wataonesha  kile  walichofanikisha, kwamba  wametatua  matatizo ya  wananchi.

Bila  hivyo  inawezekana  katika  majimbo  ya  mashariki wapiga kura  watakimbilia  katika  chama  mbadala  kwa  Ujerumani  AfD.

Nae mhariri  wa  gazeti  la Hannoversche Allgemeine  la  mjini Hannover  anaandika  kwamba  Kansela Angela Merkel  na  waziri wa fedha Olaf Scholz sasa wana  nafasi , kupitia sera muafaka za kubana  matumizi  katika  sehemu  kubwa  ya  eneo  la  kati  nchini na kunyamazisha   kile kilichoonekana  kuwa  ni ukweli katika majadiliano  yaliyokuwapo  katika  miezi iliyopita. Mhariri  anaandika.

Kwa mfano ni mara  ngapi watu wamesikia  nchini  Ujerumani maneno  kama  "hali haiwezi  kuendelea hivi"  Kila  mwananchi anaiangalia  hali  hii  kwa  njia  tofauti.  Baadhi  yao  ambao wanaona  hali  ya  kiuchumi  kuwa  nzuri , wataendelea  kupiga  kura , linasema  kundi  linalochunguza  maoni  ya  wapiga  kura, ambao wanafikia  ni karibu  Wajerumani asilimia  60. Mtazamo  wa  wale wanaosema  tuendelea  hivyo  hivyo  kiukweli  wanasema  hivyo kwa  misingi  ya upatikanaji  tu wa mahitaji ambao ndio unaowavutia zaidi.

Mzozo kati ya Uingereza  na Urusi

Nalo gazeti la  General-Anzeiger  la  mjini  Bonn  linaandika kuhusiana  na  mzozo  kati  ya  Uingereza  na  Urusi  kufuatia shambulio  la  sumu dhidi  ya  jasusi  wa  zamani  wa  Urusi  nchini Uingereza. Mhariri  anaandika.

Pande  zote mbili zinapambana , nyuma lakini  kuna  hali  ya  kuigiza ya  kutisha  ambayo haieleweki. Shambulio  dhidi ya  jasusi  wa zamani  aliyeamua  mwaka 2010  kukimbia  kutoka  Urusi  haliingii akilini. Kitu  kigani  serikali  ya  Urusi  itakipata  kwa  kufanya shambulio  hilo, siku  chache  kabla  ya  uchaguzi  ambao  Putin anawania  nchini  Urusi? Kwa  upande  mwingine  Uingereza  inataka nini , kwa  kufanya tukio  hili ambalo si la  kweli  na  kuweka  hali  ya wasi  wasi  kati  ya  Uingereza  na  Urusi, kama  vile wanavyodai Warusi.? Hakuna, mhariri  anaandika. Hali  mpya  mbaya  ya uhusiano  baridi  kati ya  mashariki  na  magharibi  inaongezeka.

Mhariri  wa  gazeti  la Stuttgerter Nachrichten  akizungumzia  mzozo huo   kati  ya  Uingereza  na  Urusi anaandika  kwamba  Imegundulika hakuna  ushahidi uliokwisha  tolewa.Mhariri  anaandika:

Kwamba  waziri  mkuu  wa  Uingereza  Theresa  May ametoa  sauti, lakini  kwa  mara  ya  kwanza  ametoa  adhabu ya hovyo hovyo  hivi.

Na  hili  hata yeye  binafsi  analifahamu.  Kutokana  na  hali  ilivyo Uingereza  pia inabidi kuwashirikisha  pia  washirika. Hii inahusu Ujerumani  pamoja  na mataifa  mengine  ya  Umoja  wa  Ulaya   na washirika  wa  NATO.  Kuna  ishara ya  wazi  kwamba  wote  wako upande wa  Uingereza, bila  kujali  Brexit. Na utayari , wa  kuimarisha vikwazo , iwapo serikali  ya  Urusi  itagundulika  kuwa  nyuma  ya shambulizi  hilo.

Chanzo. Dw.de

Urusi imewafukuza Wanadiplomasia 23 wa Uingereza

Urusi imewafukuwa wanadiplomasia 23 wa Uingereza katika hatua ya kujibu uamuzi wa Uingereza kuwafukuza wanadiplomasia wa Urusi kufuatia kashfa ya kupewa sumu kwa jasusi wa zamani wa Urusi Sergei Skripal nchini Uingereza.

UK | Nervengiftattentat auf Sergei Skripal - Ermittler in Schutzkleidung (picture-alliance/AP Photo/A. Matthews)

Urusi ambayo inadaiwa kuhusika na kitendo hicho cha kupewa sumu kwa Skripal,  siku ya Jumamosi imetangaza kuwa inawapa muda wa wiki moja pekee wanadilpomasia 23 wa Uingereza kuondoka nchni humo na kusitisha shughuli za shirika la kimataifa la Uingereza la British Council nchini humo linalohusika na masuala ya elimu pamoja na ushirikiano wa kitamaduni.

 Hayo yanajiri baada ya  Urusi kumuita hii leo balozi wa Uingereza nchini humo Laurie Bristow ambapo pia wizara ya mambo ya nchi za nje ya Urusi imeonya kuwa serikali italazimika kuchukua hatua nyingine zaidi iwapo vitendo vingine visivyo rafiki vitafanyika dhidi yake.

Urusi yajibu hatua za Uingereza

Aidha Urusi pia imesitisha shughuli za ubalozi mdogo wa Uingereza ulioko katika mji wa St Petersburg. Alhamisi wiki hii, Uingereza ilitangaza inawafurusha wanadiplomasia 23 wa Urusi kutokana na kughadhabishwa na shambulizi la sumu dhidi ya Skripal mwenye umri wa miaka 66 na binti yake Yulia mwenye umri wa miaka 33 katika mji wa Salisbury. Wawili hao wako katika hali mahututi hospitalini.

Balozi wa Uingereza nchini Urusi Laurie Bristow baada ya mkutano katika wizara ya mambo ya nje ya Urusi iliyoko mjini Moscow mnamo Tarehe 13, Machi, 2018.

Balozi wa Uingereza nchini Urusi Laurie Bristow

Urusi ambayo kesho Jumapili inafanya uchaguzi wa Rais unaotarajiwa kumpa ushindi  Rais Vladimir Putin imeonya kuwa iko tayari kuchukua hatua kali zaidi kujihami na kuilinda hadhi yao dhidi ya uhasama kutoka Uingereza na nchi nyingine za Magharibi.

Wizara ya mambo ya nje ya Urusi imesema ilitarajia Urusi kuchukua hatua za kulipiza kisasi na kuongeza kuwa Baraza la kitaifa la Usalama litakutana mapema wiki ijayo kujadili hatua zaidi itakazochukua kuhusiana na shambulizi hilo la sumu nchini Uingereza.

Katika taarifa wizara hiyo ya mambo ya nje ya Uingereza imeongeza kusema wanachokipa kipaumbele hivi sasa ni kuwahudumia maafisa wake walioko Urusi na kuwasaidia wale waliorejeshwa nyumbani.

Urusi bado haijajieleza vya kutosha

Uingereza imesisitiza kuwa hatua ilizochukua Urusi haibadilishi ukweli kuwa jaribio la kuwaua watu wawili kwa kutumia sumu lilifanywa katika ardhi ya Uingereza na hakuna shaka Urusi ilihusika na jaribio hilo.

Waziri mkuu wa Uingereza Theresa May akiwa bungeni kuwaeleza wabunge kuhusu sakata la kupewa sumu jasusi wa zamani wa Urusi Sergei Skripal mjini Salisbury, Uingereza.

Waziri mkuu wa Uingereza Theresa May

Urusi ambayo imekanusha kuhusika na shambulizi dhidi ya Skripal na binti yake imelalamika kuwa Uingereza imeshindwa kutoa ushahidi kuwa Urusi ndiyo ilihusika katika shamabulizi hilo la Salisbury na kuongeza kuwa imeshutushwa na wakati huo huo, kuchekeshwa na madai hayo yasiyo na msingi wowote na yasiyosameheka.

Siku ya Ijumaa, Waziri wa mambo ya nje wa Uingereza Boris Johnson alisema kuna uwezekano mkubwa kuwa Rais Vladimir Putin ndiye alitoa maamuzi hayo ya kumshambulia Skripal kwa kutumia sumu inayoathiri neva.

Uingereza, Marekani, Ujerumani na Ufaransa kwa pamoja zimeitaka Urusi kutoa maelezo kuhusu shambulizi hilo lililotokea tarehe 4 mwezii Machi. Wachunguzi wa Urusi wamesema wameanzisha uchunguizi wa uhalifu kuhusu jaribio la kumuua Yulia Skripal na kuongezea wako tayari kushirikiana na maafisa wa Uingereza.

Chanzo. Dw.de

Warusi wapiga kura

Warusi wameanza kupiga kura katika uchaguzi wa rais Jumapili (18.03.2018) unaotarajiwa kumpa Putin ushindi mkubwa ambao unaweza tu kuchafuliwa iwapo watu wengi hawatajitokeza kupiga kura kwa sababu matokeo yanatabirika.

Präsidentenwahl in Russland Wahllokal (picture-alliance/AP/A. Petrov)

Katika eneo  la  mashariki  mwa  Urusi, katika  mji  wa  pwani  ya  bahari  ya  Pacific wa Petropavlovsk-Kamchatsky, vituo  vya  kupigia  kura  vilifunguliwa  mapema saa  tano usiku saa  za  Urusi, na  upigaji  kura utaendelea  katika  nchi  hiyo  kubwa  hadi  vituo vitakapofungwa  katika  eneo  la  magharibi  kabisa  mwa  nchi  hiyo katika  jimbo  la Kaliningrad , masaa  22  baadaye.

Russland Präsidentschaftswahlen Nordwestrussland Nenzen (Reuters/S. Karpukhin)

Mfugaji akipiga kura yake katika maeneo ya mbali nchini Urusi.

Uchunguzi  wa maoni  ya  wapiga  kura  unampa Putin , rais  wa  sasa , uungwaji  mkono  wa kiasi  ya  asilimia  70, ama  karibu  mara  10  zaidi ya uungwaji  mkono  wa  mgombea anayemkaribia. Muhula  mwingine  utamchukua karibu  robo  karne  akiwa  madarakani, muda  mrefu  zaidi  miongoni  mwa  viongozi  wa  serikali  ya  Kremlin wapi  tu kwa  dikteta wa  enzi  wa  Kisovieti Josef Stalin.

Wengi  wa  wapiga  kura  wanamsifu  Putin, mwenye  umri  wa  miaka  65 jasusi  wa  zamani wa shirika  la  kijasusi  la  Urusi , KGB, kwa  kutetea  masilahi  ya  Urusi katika  dunia  hii yenye  uhasama, hata  kama  gharama  ni  mapambano  dhidi  ya  mataifa  ya  magharibi.

Mzozo  na  Uingereza  kuhusiana  na madai  kwamba  Kremlin ilitumia  sumu inayoathiri mishipa  ya  fahamu dhidi  ya  jasusi  wa  zamani  wa  Urusi  katika  mji mtulivu  wa  Uingereza , madai  ambayo  Urusi  inakana , haujachafua  uungwaji  wake  mkono.

Wengi  wa  wapiga  kura  hawaoni mtu mbadala  kwa  Putin, ana udhibiti  kamili  wa  medani ya  kisiasa  pamoja  na  televisheni  ya  taifa, ambako watu  wengi wanapata  taarifa  zao, na kutoa muda  mkubwa  kwa  matangazo yanayomhusu  Putin na  muda  mchache  kwa wagombea  wengine.

Präsidentenwahl in Russland Wahllokal (picture-alliance/AP/A. Petrov)

Wapiga kura wakipiga kura katika uchaguzi wa rais nchini Urusi

"Putin ndio rais  wetu. Tunajivunia," amesema  Marianna Shanina, mkaazi wa  jimbo  la Crimea. Urusi  ililinyakua  jimbo  la  Crimea  kutoka  Ukraine miaka  minne  iliyopita, na kumpa  sifa  Putin kutoka  kwa  Warusi  wengi  na  shutuma  kutoka  mataifa  ya  magharibi.

Warusi hawana mbadala kwa Putin

"Tunamtakia  ushindi  katika  uchaguzi. Familia  yetu  yote itampigia  kura Putin. Putin ! Afya njema  kwako, rais wetu  mpenzi !," Shanina  alisema  katika  mkutano  wa  kampeni  wa Putin.

Uchunguzi  wa  maoni  ya  wapiga  kura  uliofanywa  Machi 9  na  kampuni  inayomilikiwa  na serikali  ya  VTsIOM ilimpa Putin ambaye  alichaguliwa  mara  ya  kwanza  kuwa  rais  mwaka 2000, uungaji  mkono  wa  asilimia  69. Mgombea  aliyeko  karibu  nae Pavel Grudinin , mgombea  wa  chama  cha  Kikomunist , atapata  asilimia  7.

Wahlen Russland 2018 - Wahlstation - Kandidatenliste (Getty Images/AFP)

Mjumbe wa tume ya uchaguzi nchini Urusi akiweka karatasi inayoonesha picha za wagombea katika uchaguzi nchini Urusi

Mwanasiasa  wa  kwanza katika  miaka  kadhaa  kutoa changamoto  kwa  udhibiti  wa serikali  madarakani, Alexei Navalny, amezuiwa  kushiriki  katika  uchaguzi  huo  kwasababu ya  kuhumumiwa  kwa  madai  ya  rushwa, madai  ambayo  anasema  alibambikiwa na serikali.

Anatoa  wito  wa  kuususia  uchaguzi  huo, akisema  ni  kichekesho cha  kitokuwa  na demokasia, na kuwaweka  waungaji  wake  mkono  kukusanya  ushahidi  wa  mtu  yeyote atakayefanya  udanganyifu  katika  uchaguzi  kuweka  idadi  ya  juu  ya  watu  watakaoshiriki katika  uchaguzi  huo  na  uungwaji  mkono  wa  Putin.

Russland Wahlen - Alexei Navalny wird festgenommen (picture alliance/AP Photo/E. Feldman)

Kiongozi wa upinzani nchini Urusi Alexei Navalny ambaye amezuiwa kugombea katika uchaguzi huo akikamatwa na poilisi, Januari 28, 2018

Serikali  ya  Urusi pembeni  inakiri  kuwa  na  wasi  wasi kwamba  baadhi  ya   Warusi  milioni 110  wenye  haki  ya  kupiga  kura  hawatajisumbua  kupiga  kura  kwasababu  wanaamini Putin  atashinda  tu.  Uchache  wa  watu  watakaojitokeza  kupiga  kura  utaathiri  mamlaka yake  katika  muhula  ujao, ambao , chini  ya  katiba, utakuwa  wa  mwisho.

Katika  hotuba kwa  taifa  iliyotangazwa  moja  kwa  moja  na  televisheni  ya  taifa  siku  ya Ijumaa, Putin  alisema  wapigakura  wana mustakabali  wa  nchi  hiyo  katika  mikono  yao.


Chanzo Dw.de


Urusi yawafukuza wanadiplomasia 23 wa Uingereza


Serikali ya Urusi imetangaza kuwafukuza wanadiplomasia 23 wa Uingereza na imetishia kuchukua hatua zaidi ikilipiza kisasi katika mgogoro unaoendelea kukua wa kidiplomasia kufuatia shambulizi la sumu lililofanywa dhidi ya jasusi wa zamani wa Urusi nchini Uingereza.

Wizara ya Mambo ya Nje ya Urusi imesema katika tamko lake kuwa pia imeamrisha kufungwa kwa kituo cha utamaduni cha Uingereza nchini Urusi na kusitisha mkataba wa kufungua tena ubalozi mdogo wa Uingereza huko mji wa St. Petersburg.

Tayari imewaamrisha wanadiplomasia hao wa Uingereza kuondoka nchini Urusi katika kipindi cha wiki moja.

Wizara hiyo pia imemwita Balozi wa Uingereza nchini Urusi siku ya Jumamosi kabla ya kutangaza hatua hizo.

Tamko la Wizara hiyo limesema kuwa serikali ya Urusi inaweza kuchukua hatua zaidi iwapo Uingereza itaonyesha vitendo vyovyote “visivyo vya kirafiki” dhidi ya Urusi.

Hivi karibuni Uingereza iliwafukuza wanadiplomasia 23 wa Urusi baada ya Moscow kukataa kutoa maelezo vipi aina ya sumu iliyokuwa ikitumika wakati wa utawala wa Soviet iliweza kutumika katika mji wa Salisbury- Uingereza kumshambulia jasusi wa zamani wa Urusi Sergei Skripal na binti yake, Yulia.

Kulipiza kisasi kuliko tangazwa na Waziri Mkuu Theresa May katika Bunge la Uingereza kumepelekea kuanza kwa vita ya kiuchumi dhidi ya Rais wa Urusi Vladimir Putin na kikundi cha watu wachache wenye maslahi ya pamoja cha maafisa wa serikali ya Kremlin na wafanyabiashara matajiri wenye ushawishi wa kisiasa.

Vikwazo hivyo ni pamoja na kuzuia rasilmali zao ambazo wanazimiliki Uingereza pamoja na kunyimwa viza kwa watu binafsi wote waliotajwa katika sakata hilo.

Waziri Mkuu anawashinikiza washirika wa kimataifa kufuata hatua iliyochukuliwa na Uingereza na kuanza kuangaza mabilioni ya dola ambazo Kremlin imewekeza katika rasilimali zake ulimwenguni kote.

Chanzo. VOA

Thursday 8 February 2018

Tarehe sita muhimu zinazoeleza kwanini Zuma anakabiliwa na shinikizo

Rais Jacob ZumaHaki miliki ya pichaEPA

Rais wa Afrika kusini Jacob Zuma anakabiliwa na shinikizo ajiuzulu wakati wanachama wakuu wa chama chake walio na uwezo wa kumtimua wakitafakari hatua yao inayofuata.

Ameuhudumu kama rais kwa takribana thuluthi moja ya utawala wa nchi hiyo baada ya ubaguzi wa rangi, lakini uongozi wake umegubikwa kwa kashfa.

Kwa hivyo ni nini kilichotokea kutufikisha hapa tulipo? Haya ni matukio makuu.

14 June 2005: Afutwa kazi

Kwa wakati huu Zuma alikuwa naibu rais aliye na umaarufu na mkakamavu kwa miaka sita - lakini aliipoteza kazi yake baada ya kutuhumiwa katika kesi ya rushwa.

Kwa muda mrefu ameonakana kama mrithi wa rais aliyekuwepo - Thabo Mbeki.

Akiwa kijana alijiunga katika vita vya kupinga ubaguzi wa rangi katika chama cha African National Congress (ANC) na jeshi lake la chini chini kabla ya kufungwa huko Robben Island na Nelson Mandela.

Thabo Mbeki Jacob Zuma - Juni 1999Haki miliki ya pichaAFP/GETTY IMAGES
Image captionBwana Mbeki (kushoto) na Zuma baada ya hotuba yake ya kwanza bungeni mnamo 1999

Mnamo 1997, alikuwa naibu rais wa chama tawala ANC, na baadaye alitajwa kuwa naibu wa rais nchini Afrika kusini mnamo 1999.

Baadaye aligubikwa katika mzozo kuhusu biashara ya silaha yenye thamani ya $ bilioni 5 mnamo 2009 iliyohusisha kampuni kadhaa za Ulaya.

Mshauri wa fedha wa Zuma, Schabir Shaik, alipatikana na hatia ya rushwa na udanganyifu.

Katika kesi hiyo, Zuma alituhumiwa katika kesi hiyo ya rushwa na wakati amekana daima tuhuma hizo, aliipoteza kazi yake. Alishtakiwa mnamo 2007.

6 Aprili 2009: Wiki mbili

Jitihada za rais Zuma kuwania urais zilikuwa zimefika kikomo wakati waendesha mashtaka walipoamua kutomshtaki dhidi ya biashara hizo ya silaha.

Mwendesha mashtaka mkuu nchini amesema ushaihdi uliotokana na kunaswa mawasiliano ya simu unaonyesha kuwa mashtaka hayo mnamo 2007 yalichochewa kisiasa.

Upinzani mkuu waliishutumu hatua hiyo na kuitaja kuwa "utumiaji mbaya" wa jukumu la mwendesha mashtaka. Hatahivyo Zuma, ambaye wakatihuo alikuwa rais wa ANC aliishia kushinda urais wa nchi wiki mbili baadaye.

31 Machi 2016: Kidimbwi maridadi, lakini nani aliyekilipia?

NkandlaHaki miliki ya pichaGOOGLE
Image captionPicha ya satelaiti mnamo 2013 zinaonyesha ukarabati wa mkaazi ya Zuma

Mahakama ya juu ya Afrika ksuini imeamua kuwa Zuma alikiuka katiba wakati aliposhindwa kuilipa serikali pesa alizotumia kwa ujenzi wa makaazi yake binfasi.

Shirika la kupambana na rushwa lilifichua kwamba ametumia $milioni 23 katika makaazi yake Nkandla katika jimbo la KwaZulu-Natal na kujenga kidimbwi cha kuogolea na na chumba cha kutizama filamu. Baadaye alizilipa pesa hizo.

Kwa mara nyengine akakabiliwa na shinikizo la kujiuzulu. Na kwa mara nyengine hakujiuzulu.

Jacob ZumaHaki miliki ya pichaAFP / GETTY IMAGES

13 Oktoba 2017: Mashtaka yarudi upya

Mahakama ya rufaa ya juu zaidi Afrika kusini iliamua kuwa ni lazima Zuma ajibu mashtaka 18 ya rushwa, udanganyifu, na biashara haramu ya fedha yanayohusiana na biashara ya 1999 ya silaha.

Yote haya yalitokana na kesi iliyowasilishwa na chama cha upinzani Democratic Alliance katika mahakama ya Pretoria kikitaka rais akabiliwe na mashtaka. Zuma alikata rufaa, lakini alishindwa.

13 Desemba 2017: Hukumu mbili, siku mbaya

Kwanza mahakama ya Pretoria ilimuamuru Zuma aunde jopo wanasheria la uchunguzi dhidi ya tuhuma za rushwa dhidi yake na washirika wake , ambalo hatimaye aliliunda mnamo Januari.

Uchunguzi huo ni mojawapo ya mapendekezo yaliowasilishwa na tume ya kupambana na rushwa kuistisha maafisa wa serikali kuingilia kati katika kesi hiyo, hatua ambayo Zuma alijaribu kuipinga.

Jaji Dunstan Mlambo alitaja jitihada hizo za uma kujaribukuzuia hukumu kama ushauri m'baya na ukiukaji wa mfumo wa sheria.

Kisha, kwa kando, jaji mmoja aliamua kuwa rais alikiuka mfumo wa sheria kwa kujaribu kuzuia ripotikuhusu rushwa.

Takwimu zinazojitokeza katika tuhuma dhidi ya Zuma ni familia tajiri ya Kihindi kwa jina GUpta wanaotuhumiwa kutumia urafiki wao na rais kushawishi uteuzi wa mawaziri bungeni na kujipatia kandarasi za serikali.

Familia ya Gupta na Bwana Zuma wamekana makosa yoyote lakini tuhuma hizo bado zinaglipo.

18 Disemba 2017: Mrithi wa Zuma ateuliwa

Cyril Ramaphosa is one of South Africa's wealthiesHaki miliki ya pichaREUTERS

Katika ushindani wa kumrithi Zuma baada ya miaka 10 kama kiongozi wa ANC,Cyril Ramaphosa naibu rais wa Afrika kusini aliibuka mshindi. Alirithi uwenyekiti wa chama hicho katia wakati ambapo kinapoteza umaarufu chini ya utawala wa Zuma.

Alifanya kampeni kama mgombe aliye dhidi ya Zuma, na aliahidi kukabiliana na rushwa. Ushindi wake ulimueka katika nafasi ya nguvu dhidi ya rais, na kumfanya mgombea mkuu anayeweza kumrithi.

Chanzo. bbc

Hospitali mbili zapigwa mabomu nchini Syria

Majeshi ya serikali ya Syria na Mshirika wake Urusi yamezipiga hospitali mbili, jengo moja la ghorofa na sehemu zingine ambazo zililengwa na majeshi hayo katika jimbo la waasi la Idlib.

Syrien Menschen in Raqqa (Filip Warwick)

Wanaharakati leo hii Jumatatu, wameelezea kuwa mashambulio hayo yanafanyika hasa baada ya wapiganaji wa kundi la Al Qaida kuidungua ndege ya kijeshi ya Urusi mnamo siku ya Jumamosi iliyopita karibu na mji wa Saraqeb na kumuua rubani wa ndege hiyo. Na kutokea hapo mashambulio dhidi ya maeneo ya waasi yameongezeka.

Kwa mujibu wa wanaharakati wa haki za binadamu, takriban watu 23 wameuawa kutokana na mashambulizi hayo ya majeshi ya serikali ya Syria baada ya kuushambulia ngome za waasi katika vitongoji vya Ghouta Mashariki, karibu na mji mkuu wa Damascus.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa watoto wanne ni miongoni mwa wale waliouawa, Shirika linalofuatilia haki za binadamu nchini Syria lenye makao yake mjini London, Uingereza limesema watu wengine tisa wameuwawa baada ya soko lililo katika mji wa Beit-Sawa kushambuliwa.

wanajeshi wa Uturuki (Getty Images/AFP/B. Kilic)

Wanajeshi wa Uturuki

Wakati huo huo jeshi la Uturuki limesema msafara wa askari wake umeingia katika jimbo la Idlib kaskazini magharibi mwa Syria kwa ajili ya kuanzisha kituo kipya cha uchunguzi kwa lengo la kudhibiti vurugu chini ya makubaliano na Urusi. Jeshi hilo limesema kuwa kituo hicho ni cha nne kufunguliwa katika jimbo la Idlib kulingana na mazungumzo ya amani ya mjini Astana, Kazakhstan.

Idlib, ambayo kwa kiasi kikubwa inadhibitiwa na vikosi vya waasi wa Kiislamu, ipo upande wa magharibi mwa eneo la Afrin ambalo linadhibitiwa na Wakurdi ambalo linalengwa zaidi katika operesheni kubwa ya kijeshi inayofanywa na jeshi la Uturuki.

Jamii ya kimataifa imeelezea wasiwasi wake kuhusu hatima Ghouta Mashariki wakati ambapo majeshi ya serikali ya Syria na washirika wake Urusi wanaendelea kuushambulia mji huo na kusababisha upungufu mkubwa wa chakula pamoja na madawa hali ambayo imesababisha utapiamlo.

Rais wa Syria Bashar al Assad na rais wa Urusi Vladimir Putin (picture alliance/ dpa/TASS/M. Klimentyev)

Marais wa Syria Bashar al Assad na wa Urusi Vladimir Putin

Assad na washirika wake wameongeza kasi katika vita hivyo vya miaka saba, na wameweza kuyateka maeneo kadhaa na kuwafurusha waasi kutoka kwenye maeneo mengi na miji mikubwa, hali iliyoyalazimisha baadhi ya makundi kujisalimisha mnamo mwaka jana.

Wakati hayo yakijiri Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan alikutana leo hii na kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis katika mji wa Vatican. Polisi walikuwa na kibarua kigumu cha kuwadhibiti  waandamanaji wakati ambapo hisia zinaendelea kuwa kali kutokana na operesheni ya Uturuki dhidi ya wanamgambo wa Kikurdi ndani ya Syria. Papa Francis alimpa Erdogan kisanamu kilichokuwa na picha ya malaika anayemkaba shetani  - ikiwa ni ishara ya kukumbushia amani na haki.

Mwandishi: Zainab Aziz/APE/AFPE

Mhariri: Gakuba Daniel

Chanzo. Dw.de


 
 
Blogger Templates